Facebook LIKE

Tuesday, July 10, 2012

Yanga yaichapa JKT Ruvu kuelekea michuano ya Kagame

Mabingwa wazamani wa Tanzania,Dar Young Africans wameichapa timu ya JKT Ruvu 2-0 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Ukiwa na mchezo wa kwanza wa kirafiki kwa kocha mpya wa klabu hiyo Mbeligiji,Tom Saintfiet.

Yanga ambayo inajiandaa na michuano ya Kagame ambayo inaanza wikiendi hii walijipatia mabao yake kupitia beki wake kisiki wa kati,Nadir Haroub"Cannavaro" katika dakika ya 18.Hadi mchezo huo unaenda mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao hilo moja.Katika kipindi cha pili Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa kiungo Nizar Khalfan na nafasi yake kuchukuliwa na mshambuliaji mganda Hamis Kiiza,ambaye katika dakika ya 73 ya mchezo huo aliipatia Yanga bao la pili.

Katika pambano hilo Kikosi cha Yanga kilikuwa hivi;

1.Yaw Berko - 19
2.Juma Abdul - 14
3.David Luhende - 29>>Idrissa Rashid-12
4.Nadir Haroub 'Cannavaro' (C) - 23
5.Kelvin Yondan 'Vidic' - 5
6.Athuman Idd 'Chuji' - 24
7.Haruna Niyonzima - 8>>Shamte Ally-15
8.Rashid Gumbo - 16
9.Said Bahanunzi - 11>>Stephano Mwasika-3
10.Jersyon Tegete - 10
11.Nizar Khalfan - 7>>Hamis Kiiza-20

No comments:

Post a Comment