Facebook LIKE

Tuesday, November 6, 2012

Huyu ndo mtangazaji anayekuja kwa kasi Bongo mwenye ndoto za kuja kuwa......!!


  •  Ana ndoto za kufika mbali katika utangazaji Bongo
  • Afunguka na kusema anavutiwa na utangazaji wa Big Tiger na Ezden
  • Pia anawakilisha kundi maarufu la WAKACHA
HUYU NDO ABBA MOKO


Abbas Yussuph,21,ana dream ya kuwa Big Tigger wa baadae hapa +255 (Tz) kwenye suala la utangazaji,Abbas maarufu kwa jina la utangazaji ‘’Abba Moko’’ ni mwanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari(DSJ) aki-persue Dipolma in Jornalism,anamapenzi makubwa na suala la utangazaji na kwa sasa anashikilia cheo cha muingizaji sauti ya matangazo ya bush hapo chuoni kwake na kuendesha bush hizo az a hoster, pia ni ripota wa entertainment newz @BarmedasTv ya jijin Mwanza. "Huu ni mwanzo mzuri wa kufikia ndoto zangu za kuwa bonge la mtangazaji na  muendeshaji wa matamasha makubwa hapa Tanzania’’
 Kama ilivyo kwa watu wengi, Abba Moko nae ana mtu anayemuangalia kama kioo chake,’’I have been idolizing one of the hottest presenter in Tanzania, Ezden The Rocker wa Kiss Fm."

Ezden Jumanne"Ezden The Rocker" kushoto

"Napenda anavyohost vipindi vyake na  anavyojiweka kinidhamu akiwa kwenye kipindi",anafunguka Abba. Lakini pia ukitoka nje ya Tz land kuna mtu ambaye Abba anampenda na hapa ni moja kwa moja tunashuka pale kwa Obama Marekani, BET na tunamuangalia jamaa anaejiita Big Tigga ambaye ni mtangazaji na muendeshaji wa vipindi vya BET
BIG TIGGER NA ABBA MOKO



Pia ukiachilia mbali na suala la utangazaji Abba anapenda sana kuwa muandaaji(producer) wa vipindi mbali mbali pamoja na graphit design.’’Sitaki niwe mtu hasiyejua vitu vingi kwenye fani yangu ya utangazaji kwahiyo napenda sana niwe producer wa vipind na matangazo pamoja na graphit design, kwa hiyo mwakani ntapiga shule kuhusu hizi mambo hapo kwa majiran zetu Kenya na very soon naachia ma program goes by de name’’Freestyle Session’’ ni cha mambo ya freestyle kwa undergroundz wakal ambacho kitakuwa kinarushwa kupitia blog yangu SWAGG ZA KITAA kwahiyo fanz wangu na raia wote get ready 4dat’’, ndivyo alivyomalizia kijana huyo mwenye migogo na swagga za kikaka zaidi.Pia Abba Moko ni member wa kundi la muziki lijulikanalo kama ‘’THE SWITCH’’ linaloundwa na Gyan Bobic,Joshy Joh na Abba Moko mwenyewe na kundi hilo lipo ndani ya kundi maarufu la WAKACHA WARRIORS under Flow Ze Banks ,Cyrill"KAMIKAZE" na Jux Vuitton kwahiyo kwa pamoja wanatengeneza kundi linaloitwa (TSWW)
Kutoka kushoto ni Kricha,Jux,Cyrill,GiggaFlow,AbbaMoko,JoshyJoh na GyanBobic
GYAN BOBIC,ABBA MOKO(katikati)na JOSHY JOH
WAKIWAKILISHA KUNDI LA"THE SWITCH"
Kundi hilo are in de booth ready kwa kupika mkwaju mkali waliomshirikisha Flow,Kricha na C.E.O wao Cyrill Kamikaze,na pia kwa xaxa limeachia tshirt zao zinazojulikana km #TEAM DE SWITCH,fashion on fashion..code on code ambazo zimeonekana kufanya vizur kwa raia wengi na funz wao pia.
T-SHIRTS ZA "TEAM DE SWITCH"

T-SHIRTS ZA #TEAM DE SWITCH PIA ZIPO SOKONI 
KWA WANAOHITAJI T-SHIRTS HIZI WASILIANA KWA NAMBA HII +255654781281 au cheki na Facebook hii>>Abba Moko


Sunday, September 23, 2012

Do you know that this Rapper will quit Rapping in order to be a Pornstar




Mystikal is giving music one last shot — but tells TMZ, if he fails to make another hit on his next album … HE’S TURNING TO PORN.
This is not a joke. Mystikal tells us, he needs to make sure the money keeps coming in … and if there’s one thing he’s good at, it’s having filthy sex. So porn is his plan b.
Which is either crazy … or perfect — because Mystikal served SIX YEARS in prison for sexual battery beginning in 2004 after forcing his hairstylist to perform sex acts on him.
But Mystikal is undeterred, telling us he already has a history in porn — winning an AVN award in 2003 for an adult movie he made (he doesn’t actually have sex in it though).
We asked Mystikal who he’d want to star in his first skin flick, and the rapper said Pinky — adding, “She’s a bad bitch. I would take her down in a second.”
As for whether he’s got the requisite hardware to be a male porn star, Mystikal wouldn’t give an exact size, but said, “I’m definitely the man, the myth, and the legend.”

Huyu ndo msichana ambaye amefananishwa na Kim Kardashian inasemekana ameigiza video ya ngono na rapper Kanye West







Saturday, September 1, 2012

MAKALA:Mbwana Samatta;"Realmadrid walinifuata Kinshasa."(Imeandikwa na Edo Kumwembe)

EDO KUMWEMBE, ALIYEKUWA LUBUMBASHI
NI swali linalowaumiza Watanzania wengi.

Je, Samatta anaweza kuuzwa kwenda kucheza Ulaya?
MBWANA SAMATTA
Watanzania wanatamani kumuona Samatta akiendeleza ndoto zake licha ya sasa kuwa staa wa TP Mazembe.
Wengi wangetamani kumuona akicheza moja kati ya ligi kubwa barani Ulaya, iwe Hispania, England, Ufaransa, Italia au Ujerumani.

Nikiwa na Samatta tukielekea katika sehemu moja ya chakula cha mchana kinachopikwa na Watanzania inayoitwa Parachute, Samatta anaonekana kuwa na hisia zile zile za Watanzania.

"Bado nina kiu ya kucheza Ulaya.

Mimi hapa naona napita kwa sababu natamani sana kukipiga Ulaya.

Najua Watanzania wanachotaka na mimi bado sijabadili msimamo wangu, nikipata nafasi ya kucheza Ulaya tu namlilia Moise Katumbi.

Mtu mwenyewe anaonekana kuwa na huruma kidogo," anasema Samatta huku Thomas Ulimwengu akicheka.

Hili la Katumbi ndilo linaonekana kuwa kikwazo kikubwa katika mazungumzo. Hata Samatta mwenyewe anakiri kwamba Katumbi ni tatizo kubwa kwake kuuzwa Ulaya.

"Nimezungumza na Katumbi kuhusu mimi kucheza Ulaya lakini anaonekana hataki kabisa kusikia habari za mimi kuuzwa.

Kuna wakati aliniambia wazi wazi kwamba timu inayonitaka lazima iilipe Mazembe kiasi cha Euro 10 milioni.

Mimi sina thamani hiyo na wala sidhani kuna mchezaji anayecheza Afrika ana thamani hiyo.

"Nadhani hapo nia yake ni kutoniuza. Eti brother, haiwezekani timu itoe Euro 10 milioni kwa ajili yangu.

Nadhani nikimwambia kuwa nataka kuhama lazima kutakuwa na kasheshe," anasema Samatta huku akicheka.

Hata hivyo, Samatta ananishangaza zaidi anaposema kuwa kuna ofa za kutoka Ulaya zimeshafika mezani kwa Katumbi kwa ajili yake.

Ananishangaza zaidi anaposema kuwa hata wababe wa Hispania, Real Madrid walishatuma maskauti wao wamtazame.

"Katumbi aliwahi kuniambia kuwa maskauti wa Real Madrid walisafiri kuja kunitazama wakati tunacheza na Vita katika Ligi Kuu yetu hapa Congo.

Ilikuwa mechi tuliyocheza Kinshasa, lakini siku ile mimi sikucheza vizuri kwa hiyo sidhani kama walivutiwa au vipi," anasema Samatta.

Pamoja na hali hiyo, Samatta anakiri kwamba ili mchezaji wa Mazembe atimize ndoto zake za kucheza Ulaya ni lazima akubali kuona kipato chake cha pesa kinapungua, labda kama akisajiliwa na timu kubwa barani Ulaya.

"Hata hivyo, braza ukihama Mazembe kwenda Ulaya inabidi uende timu inayoeleweka, kama ukienda timu ya kawaida pato lako litapungua sana kwa sababu Mazembe inalipa posho nzuri kuliko hizo timu za Ulaya.

"Unamuona huyu Kabangu (kiungo wa Mazembe aliyeuzwa kwenda Anderlecht misimu miwili iliyopita) amerudi hapa na ameniambia amerudi kwa sababu hapa wanalipa vizuri kuliko Anderlecht. Yupo hapa nadhani unamuona ameshaongea na Katumbi na ameanza mazoezi.

"Hapa tukishinda mechi kama hizi za kimataifa katika Ligi ya Mabingwa, Katumbi anaweka dola laki tatu mezani (Sh 450 milioni). Tunakuwa watu kama 25 na tunagawana pesa zote hizo.

Sasa kwanini tusiendeshe magari haya? Nadhani kuna klabu za Ulaya hazijafikia posho hizi.

"Hata Katumbi mwenyewe amewahi kuniambia kuwa nikitoka hapa kama naenda Ulaya inabidi niende kucheza timu kubwa iliyo juu ya Mazembe hata kwa mapato."

Kwa fedha alizonazo Katumbi, ambaye pia ni Gavana wa Jimbo la Katanga, huku mara zote akiwa anaonekana katika televisheni akifanya shughuli mbalimbali za Serikali, namuuliza Samatta kama huwa anapata muda wa kuzungumza na Katumbi.

"Huwa ananipigia simu mara nyingi. Lakini mpaka yeye awe na jambo lake au ajisikie. Katumbi ana mambo mengi, mara utasikia yuko Ubelgiji mara kesho asubuhi unamuona Lubumbashi.

Mimi nikimpigia simu haipokelewi, inaita tu. Halafu anaweza kunipigia hata saa nane usiku. Ni mtu mkubwa sana hapa."

Baada ya muda tunaenda Western Union ambapo Samatta anatuma pesa kwa baba yake nyumbani Tanzania.

Ni kiasi kikubwa cha fedha, lakini huo unabakia kuwa utaratibu wake wa kila mwezi.

"Huwa natuma fedha nyumbani kila mwisho wa mwezi.

Ni kitu cha kawaida, Mzee Samatta lazima ajivunie kuwa na mwanaye au vipi braza? Ndiyo maisha yalivyo, tunapata baraka za wazee."

"Hawa wachezaji wa Zambia kina Kalaba, Sunguluma, Sinkala ikifika mwisho wa wiki wanaendesha magari yao kwenda hapo Ndola, si mbali ni mwendo wa saa moja tu, mimi na Thomas (Ulimwengu) inabidi tutume fedha tu nyumbani kwa sababu hatuna uwezo wa kurudi Tanzania mara kwa mara."

Asubuhi ya siku ambayo natakiwa kuondoka inafika. Lakini wote watatu, mimi, Samatta na Ulimwengu tunafunga mabegi.

Wao mabegi yao yanalazimika kusafiri kwa basi kwenda Ndola ambako timu itaweka kambi, lakini wachezaji watasafiri jioni kwenda huko na ndege yao binafsi.

Tunafika mpaka mazoezini kwa ajili ya kuwaacha na kisha nichukue gari la Samatta kupelekwa uwanja wa ndege kuwahi ndege ya saa nne asubuhi.

Tofauti na siku nyingine, safari hii hatupaki ile sehemu ambayo Samatta huwa anapaki gari mazoezini. Hii ni kwa sababu Mfalme Mputu anaweza kutuzuia na nikachelewa kwenda uwanja wa ndege.

Thursday, August 30, 2012

Mbuyu Twite atua rasmi Jangwani



Mbuyu Twite (mwenye jezi ya njano) 
Twite, Twite, Twite!!!!
Hayo ni maneno ya washabiki wa Yanga walikua wakiimba kumshangilia Twite mara baada ya kutua Uwanja wa Ndege wa mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
Hakika ilikuwa ni furaha, vifijo na nderemo kwa watu waliofurika kumpokea mchezaji wao mpya Mbuyu Twite. 
Mbuyu Twite akiwa na katibu mkuu wa Yanga, Mwesigwa Selestine
Mchezaji mpya wa kimataifa wa timu ya taifa ta Rwanda ,Mbuyu Twite amewasili leo jijini Dar kutokea nchini Rwanda tayari kujiunga na mabingwa wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati timu ya Young Africans.
Twite aliwsali majira ya saa 10:15 kwa majira ya Afrika Mashariki kwa shirika la ndege la Rwanda Air na kupokelewa na viongozi wa Young Africans na washabiki wengi waliojitokeza kumpokea Uwanja wa ndege wa Mwl JK Nyerere.
Mara baada ya kuwasili mlango wa kutokea watu mashuhuri, Twite alipewa jezi ya Yanga yenye namba 4 mgongoni iiiliyoandikwa jina la Aden Rage, mwenyekiti wa Simba. 
Umati mkubwa ulijitokeza kiasi kilichopelekea Twite kushindwa kutokea mlango wa kawaida wa kupelekea uongozi wa uwanja huo kumuongoza Twite kutokea mlango wa wageni mashuhuri.
Msafara ulianza Uwanja wa ndege wa Mwl JK Nyerere kuelekea makao makuu ya klabu, huku magari yakiwa mengi, pikipiki na wengine wakitembea kwa miguu mpaka makao makuu ya klabu. 
Msafara uliendelea mpaka makao makuu ya klabu, kwa kupitia mtaa wa msimbazi ambapo wapenzi na washabiki wa simba hawakuweza kuamini macho yao mara baada ya kumuona Twite akiwa katika gari ndogo ya Yanga, na washabiki na wanachama wakiwazomea simba na kuwakejeli kwa maneno ya dhihaka.


Umati uliojitokeza kumpokea Mbuyu Twite, Uwanja wa Mwalimu JK Nyerere
Mara baada ya kufika makao makuu ya klabu ya Yanga, mchezaji Mbuyu Twite alipanda juu ghrorofani kuwasalimia washabiki na wanachama waliojitokeza kumpokea, kisha alikabidhiwa funguo ya chumba ambacho atakua akikitumia kwa kipindi chote atakachokuwa Yanga.
Mbuyu Twite amesema anajisikia vizuri, na furaha na mwenye bahati kuja kuchezea timu ya Yanga na anawaahidi kuonyesha kiwango cha juu kipindi chake chote atakaoitumikia Young Africans, Twite kesho anatajumuika na wenzake katika mazoezi asubuhi Uwanja wa Loyola kabla ya jumamosi kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Coastal Union.

Wednesday, August 29, 2012

Magoli ya mechi ya RealMadrid dhidi ya Barcelona haya hapa kama ulikosa mechi RealMadrid 2-1 Barcelona

Hili ni Goli la kwanza lililofungwa na Gonzalo Higuain wa RealMadrid

Gonzalo Higuaín goal(Real Madrid vs Barca 2nd leg supercup)Twitter @TheKSTYLES from Kelly Kelvin
on Vimeo.
Hili ndilo goli alilofunga Cristiano Ronaldo ambalo limeiwezesha RealMadrid kubeba kombe la kwanza msimu huu ni kombe la SuperCup linalokutanisha bingwa wa LIGI(RealMadrid) na bingwa wa KOMBE LA MFALME(Barcelona).Mechi ya kwanza Barca walishinda 3-2 nyumbani kwao ila ugenini wamefungwa 2-1 kwahiyo RealMadrid wamebeba kombe hilo kwa faida ya mabao ya ugenini

Real Madrid Vs Barcelona 2-1 Cristiano Ronaldo Fantastic Goal Spanish Super Cup 29-082012 (2nd leg)Twitter @TheKSTYLES from Kelly Kelvin on Vimeo.
HIGHLIGHTS ZA MABAO YOTE HII HAPA

2-1 Real Madrid highlights win its ninth Supercup Twitter @TheKSTYLES from Kelly Kelvin on Vimeo.

Wednesday, August 22, 2012

Video ya Marley ft. Belle9-Sina cha Kupoteza.Bonge la track hebu cheki


Marley ft. Belle9-Sina cha kupoteza from Kelly Kelvin on Vimeo.

Baadhi ya picha za duka la linalomilikiwa na rapper Soulja Boy alilolifungua hivi karibuni..!!

RAPPER TWISTA ALIJITOKEZA KUMSAPOTI SOULJA BOY 
BUN_B NAE ALIJITOKEZA KUMPA SAPOTI SOULJA BOY
SOULJA BOY AKIWA KATIKA DUKA LAKE
SOULJA BOY AKIWA NA MMOJA YA MASHABIKI WAKE KWENYE DUKANI LAKE
Add caption
BAADHI YA WATU WALIOJITOKEZA KWENYE DUKA HILO
SOULJA BOY AKIWA NA MASHABIKI WAKE
TUNECHI(LilWayne) nae
soulja boy


Na hichi ndicho alichokiandika kwenye Twitter account yake SOULJA BOY

Na kama upo Twitter waweza Kutufollow pia kupitia hapa;

Mshindi wa shindano la Bibi Bomba huyu hapaa....!!



 Shindano ambalo lilikuwa likionyeshwa na kuandaliwa na Clouds Media Group kupitia kituo chake cha CLOUDS TV.Ambapo baadhi ya mabibi walikusanywa na kuwekwa pamoja huku kila mmoja akionyesha kipaji,ufundi na utundu alionao na bibi aliyeibuka kidedea ndo kama unavyomuona hapo chini;
Veronica Mpangala  a.k.a Tukinao

Monday, August 20, 2012

Kigamboni ya miaka ijayo....!! Itakuwa kama hivi....!!Hebu cheki kama haukuiona hii


THE KIGAMBONI NEW CITY PLAN(Official) from Kelly Kelvin on Vimeo.

Yanga yaichakaza African Lyon katika Uwanja wa Taifa....!!


KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA AFRICAN LYON
Mabao yaliyowekwa wavuni na Haruna Niyonzima,Simon Msuva,Jerry Tegete na moja la kujifunga yalitosha kuipa ushindi wa mabao 4-0,Mabingwa wa Kombe la Kagame,Yanga katika mchezo wa kirafiki dhidi ya klabu ya African Lyon.Katika mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Taifa,Dar es salaam.

Yanga walianza kuhesabu mabao hayo katika dakika ya 8 ambapo mabeki wa African Lyon wakiwa katika harakati za kuokoa mchumo ulioelekezwa langoni kwao walijikuta wakijifunga wenyewe,Hadi mapumziko Yanga walikuwa wanaongoza kwa goli hilo moja.
SHAMTE,KAVUMBAGU,TEGETE na MSUVA
Katika kipindi cha pili cha mchezo huo Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa Hamis Kiiza na nafasi yake kuchukuliwa na Jerry Tegete.Mabadiliko hayo yalionekana kuisaidia Yanga na ndipo katika dakika ya 54 kiungo mchezeshaji Haruna Niyonzima alipoipatia Yanga bao la pili kwa njia ya mkwaju wa penati baada ya madhambi kufanyika katika lango la African Lyon.Katika dakika ya 72 mshambuliaji mpya chipukizi wa Yanga,Simon Msuva aliipatia Yanga bao la tatu kabla ya Jerry Tegete kukamilisha idadi ya mabao manne katika dakika ya 90 ya mchezo huo.
SIMON MSUVA AKISHANGILIA BAO ALILOFUNGA
Kikosi cha Yanga kilikuwa hivi:

Gazeti La Ijumaa>>Unafiki wa Wema Sepetu na Snura.Kisa ni...!!

http://api.ning.com/files/-xhPZ98Kq7naU4FFcReIiALFoGdWOAilKJUB-w9AWqD8WimuhkfJ-5zodXhv2iPTBKUqpP3pBieSWphQctsTvYvNOdfpYg7x/UZINDUZIWAFILAMUYA8.JPG
WEMA NA SNURA
USHOSTITO wa Wema Sepetu na Snura Mushi uliodumu kwa miezi kadhaa umeraruliwa ukidaiwa kuvunjika kwa kuwa ulikuwa wa kinafiki kutokana na kuvunja kiapo walichokula runingani kuwa hatawaachana, Ijumaa Wikienda limejazwa werawera na wabaya wao.
MTU WA KARIBU ATIRIRIKA
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao, Wema na Snura walikuwa marafiki vinyonga kwani kila mtu alijua muda siyo mrefu watasalitiana na kuanza kuvujisha siri zao na hicho ndicho kilichotokea.
KISA NI NINI?
Kwa mujibu wa chanzo hicho, Wema alidai kuwa Snura amemsema vibaya kwa ndugu zake na kutangaza kwa wanahabari kuwa amerudiana na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, jambo ambalo lilimchukiza.
Chanzo kilitiririka kuwa baada ya urafiki huo kuvunjika, Wema alimnyang’anya Snura vitu vyote ambavyo alikuwa amemnunulia na kuanzia hapo mawasiliano baina yao yalikatika.
“Snura ameamua kuvunja kile kiapo alichokula runingani kwa machozi, sasa sijui atapata wapi yale mawigi aliyokuwa akipewa na Wema?,” kilihoji chanzo na kuingia mitini.
SNURA ANASEMAJE?
Alifunguka: “Mimi sijui sababu ya urafiki wetu kuvunjika kwa sababu Wema hajaniambia, angekuwa ni mtu mwenye akili na busara angenieleza.”
NYUMBANI KWA WEMA
Ili kupata mzani wa habari hiyo, Ijumaa Wikienda lilimpigia simu Wema lakini haikupokelewa hivyo likatimba nyumbani kwake ambapo wakiongozwa na Vincent Kigosi ‘Ray’, wasanii hao walitumia nafasi yao kumkashifu mwandishi wetu kwa maneno mabaya yasiyoandikika gazetini, tunayafanyia kazi.

Friday, August 10, 2012

Huyu ndo msanii wa kwanza kusign kwaajiri ya shoo za FIESTA 2012 Bongo...!!

Kila mwaka matamasha makubwa ya Fiesta huwa yanafanyika nchi ikiwa ndo yanaelekea kuanza kwa matamasha hayo ambayo hufanyika nchi.Huyu ndo msanii wa kwanza wa Kibongo kusign kwaajili ya kufanya shoo hizo za FIESTA 2012
SHETTA
Baada ya kusign Shetta aliandika kwenye account yake ya BBM kuwa;

Thursday, August 9, 2012

Video ya Agnes Masogange ya ngono hii hapa...!!Tunaomba radhi kwa watakao kereka nayo.


  • Tunaomba radhi kwa watakao kereka nayo.
  • Kama haikufai usiitazame


Friday, August 3, 2012

Huu ulikuwa ujumbe kwa wale watumiaji wa mtandao wa Twitter wenye nia ya account zao kuwa "VERIFIED"kwenye Twitter..!!


Ngoma mpya ya Dogo Janja ft PNC-Ya moyoni.Download na sikiliza hapa.


Wednesday, August 1, 2012

Mrisho Ngassa asema hajui chochote kuhusu Simba na hatojiunga na timu hiyo..!!


Ngassa ameuzwa Simba kama kiroba cha mchele,Azam hawajaongea na Ngassa pia Ngassa mwenyewe hajaongea na Simba juu ya huu uhamisho. Namnukuu ' mimi sina Taarifa official za kuuzwa Simba,sijafanya mazungumzo na azam pamoja na Simba juu ya uhamisho,kifupi Sitajiunga na Simba ! Nimemaliza kumnukuu Mrisho Ngassa.

Monday, July 30, 2012

Sikiliza ngoma mpya kali ya Kelly Rowland ft. Lil Wayne-Ice.Wawili hao wamefanya collabo nyingine baada ya ngoma ya motivation


Video ya Ney wa Mitego-Nasema nao,hii hapa..!!



Azam FC wamweka Mrisho Ngassa sokoni rasmi hii ndio bei na sababu za kumweka winga huyo sokoni



MRISHO NGASSA BAADA YA MECHI YA FAINALI KOMBE LA KAGAME

Klabu ya Azam FC inapenda kutoa taarifa rasmi kuwa milango iko wazi kwa klabu yoyote kumnunu mchezaji Mrisho Ngassa kwa gharama ya $ 50,000.

Azam FC imefikia hatua hiyo baada ya mchezaji huyo kuonyesha kutokuwa na mapenzi na klabu hiyo na badala yake kuipenda klabu aliyotoka ya Yanga.
Hivyo uongozi wa klabu unapokea maombi kwa klabu yoyote inayomuhitaji mchezaji huyo.
Azam FC ilitoa nafasi ya upendeleo kwa klabu ya Yanga lakini hakuna ofa iliyoletwa kuhusu, klabu imepokea ofa kutoka Simba kumuhitaji mchezaji huyo.

Ngassa anauzwa siku chache baada ya kukubali kuvaa jezi ya Yanga na kuibusu logo ya timu hiyo, baada ya kumalizika kwa mchezo wa nusu fainali kati ya Azam FC na AS Vita Club ya Congo DRC katika mashindano ya Kombe la Kagame yaliyomalizika Julai 28 mwaka huu.

Sunday, July 29, 2012

Mshindi wa shindano la Tusker Project Fame 5 huyu hapa..!

MKENYA,RUTH MATETE
Anaitwa Ruth Matete kutoka Kenya na ndio ameondoka na kitika cha million 5 za kenya na mkataba wa kurecord album wenye thamani ya million 10.Ruth ana miaka 26 na amewashinda vijana wa nne wenye uwezo mkali sana ambao ni Joe kutoka burundi ndio namba nne ,akifatiwa na Jackson kutoka Rwanda , Doreen kutoka Kenya akiwa namba mbili . Wakati wanataja washindi mtangazaji wa tusker project fame aliwabakiza wawill Ruth na Doreen aka Miss Probation na kuacha watu wakitabiri yupi atakuwa mshindi . Shindano hili huwa linaanza na washindani 15 na 11 hutolewa mapema kabla ya week ya fainali
Usiku wa fainali, Kundi la vijana wakali kupitia ngoma zao kama party don't stop na Hold it down Camp Mulla walifanya show na Sarakasi dancers.Show ya Camp Mulla ilikuwa nzuri ila malalamiko ya watazamaji ni mavazi na muonekano wa Camp Mulla haujaendana na show hio.

Beats kali kutoka K-Styles entertainment contact us for acquirements/needs

Sunday, July 22, 2012

Hii hapa ndo aina ya ndege ambayo Wakenya wamepewa na Marekani katika kupambana na AL SHABAB

Taarifa kutoka Marekani zinaeleza kuwa Wizara ya Ulinzi ya Marekani itaipatia Kenya ndege nane ndogo zisizohitaji rubani, ikiwa ni sehemu ya msaada wa kijeshi kwa nchi za Afrika Mashariki, ili kuzisaidia kupambana na wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, al-Shabaab.
Ndege isiyobeba rubani, drone
HII NDEGE HAITUMII RUBANI NA NI YA KUPELELEZA ZAIDI
Gazeti la Wall Street Journal la Marekani limearifu kuwa Kenya itapata ndege hizo ambazo hazitakuwa na silaha, lakini zinaweza kugundua maeneo yanayofaa kulengwa na ndege au majeshi ya ardhini.
Gazeti hilo limesema ndege zisizokuwa na rubani ni sehemu ya msaada wa Marekani, pamoja na malori, zana za mawasiliano, na silaha kwa Burundi, Djibouti na Uganda.

Saturday, July 21, 2012

Wale wapenzi wa Movie na ChrisBrown hii hapa Trailer ya Battle of the year(3D)


  • Battle of the Year stars Josh Holloway (Lost), Chris Brown (Takers), Laz Alonso (Jumping the Broom, Avatar) and Josh Peck (The Wackness).

Ngoma mpya ya Barnaba-Sijutii kwa niliempata,download na sikiliza hapa