Facebook LIKE

Monday, August 20, 2012

Yanga yaichakaza African Lyon katika Uwanja wa Taifa....!!


KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA AFRICAN LYON
Mabao yaliyowekwa wavuni na Haruna Niyonzima,Simon Msuva,Jerry Tegete na moja la kujifunga yalitosha kuipa ushindi wa mabao 4-0,Mabingwa wa Kombe la Kagame,Yanga katika mchezo wa kirafiki dhidi ya klabu ya African Lyon.Katika mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Taifa,Dar es salaam.

Yanga walianza kuhesabu mabao hayo katika dakika ya 8 ambapo mabeki wa African Lyon wakiwa katika harakati za kuokoa mchumo ulioelekezwa langoni kwao walijikuta wakijifunga wenyewe,Hadi mapumziko Yanga walikuwa wanaongoza kwa goli hilo moja.
SHAMTE,KAVUMBAGU,TEGETE na MSUVA
Katika kipindi cha pili cha mchezo huo Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa Hamis Kiiza na nafasi yake kuchukuliwa na Jerry Tegete.Mabadiliko hayo yalionekana kuisaidia Yanga na ndipo katika dakika ya 54 kiungo mchezeshaji Haruna Niyonzima alipoipatia Yanga bao la pili kwa njia ya mkwaju wa penati baada ya madhambi kufanyika katika lango la African Lyon.Katika dakika ya 72 mshambuliaji mpya chipukizi wa Yanga,Simon Msuva aliipatia Yanga bao la tatu kabla ya Jerry Tegete kukamilisha idadi ya mabao manne katika dakika ya 90 ya mchezo huo.
SIMON MSUVA AKISHANGILIA BAO ALILOFUNGA
Kikosi cha Yanga kilikuwa hivi:
1.Yaw Berko,2.Shadrack Nsajigwa(G.Taita dk.75),3.Oscar Joshua(S.Mwasikia dk.79),4.Nadir Haroub 'Cannavaro'(Ibrahim Job dk.85),5.Kelvin Yondani(Ladislaus Mbogo dk.63),6.Athuman Idd Chuji(Frank Dumayo dk.58),7.Saimon Msuva(Omega Seme dk.89),8.Haruna Niyonzima(Rashid Gumbo dk.77),9.Didier Kavumbagu(Idrissa Rashiddk.85),
10.Hamis Kiiza(J.Tegete dk.45),11.David Luhende(Shamte Ally dk.63)

No comments:

Post a Comment