Facebook LIKE

Tuesday, July 17, 2012

Yanga yafanya mauaji Kagame yawapiga Wasudan goli 7


Mabao yaliyotiwa kimiani na washambuliaji Mganda Hamis Kiiza,Said Bahanuzi na kiungo Nizar Khalfan yameiwezesha klabu ya Yanga kuibuka na ushindi wa goli 7-1 dhidi ya timu ya Waw Salaam ya Sudan.

Katika mchezo huo ulitawaliwa zaidi na Yanga mshambuliaji Said Bahanuzi ndiye aliyeipatia Yanga bao la kuongoza katika dakika ya 12.Dakika tano baadae Bahanuzi tena alitumbukiza mpira kimiani na kuipatia Yanga bao la pili katika dakika ya 17.Mshambuliaji Mganda Hamis Kiiza alianza kuhesabu mabao yake manne aliyofunga katika pambano hilo katika dakika ya 18,25,30 na 35.Hadi timu hizo zinaenda mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa mabao 6-0.

Katika kipindi cha pili Yanga waliwatoa Kevin Yondan,Haruna Niyonzima na Stephano Mwasika na nafasi zao kuchukuliwa na Juma Seif,Rashid Gumbo na Idrissa Rashid.Katika dakika ya 75 kiungo Nizar Khalfan aliipatia Yanga bao la saba.Waw Salaam walijipatia bao lao katika dakika ya 90 ya mchezo

Katika mchezo huo kikosi cha Yanga kilikuwa hivi;

1.Yaw Berko - 19
2.Godfrey Taita - 17
3.Oscar Joshua - 4
4.Nadir Haroub "Cannavaro" (C) - 23
5.Kelvin Yondani "Vidic" - 5>>>Juma Seif"Kijiko"-13
6.Athuman Idd Chuji - 24
7.Nizar Khalfan - 7
8.Haruna Niyonzima - 8>>>Rashid Gumbo-16
9.Said Bahanunzi - 11
10.Hamis Kiiza - 20
11.Stephano Mwasika - 3>>>Idrissa Rashid"Messi wa Jangwani"-12

No comments:

Post a Comment