Facebook LIKE

Tuesday, May 29, 2012

Tetesi za Usajili Bongo hizi hapa,Unaijua bei ya kumng'oa Okwi Msimbazi..?Hii hapa........

1.Golikipa Mghana wa Yanga kubaki Jangwani mara baada ya kuongeza mkataba na klabu hiyo ya Yanga.

2.Imefahamika kuwa kiungo wa zamani wa klabu ya VancouverWhiteCaps,NizarKhalfan ameitosa klabu ya Simba na kuamua kujiunga na mabingwa wa zamani Yanga,pia inasemekana amesaini mkataba wa mwaka mmoja na Yanga.

3.Simba yaachana na JerryTegete,klabu ya Simba imesitisha mpango wake wa kumsajili mshambuliaji wa Yanga JerryTegete baada ya kusemekana kuwa mchezaji huyo ana mapenzi zaidi na Yanga hivyo wana wasiwasi kama ataweza kuitumikia Simba vizuri.

4.Yanga kuibomoa MtibwaSugar,klabu ya Yanga ipo kwenye hatua ya kuwasajili wachezaji watatu kutoka Mtibwa kwa mpigo.Wachezaji hao ni washambuliaji SaidiBahanuzi na HusseinJavu pamoja na beki wa kulia chipukizi JumaAbdul.Pia inasemekana Yanga itajaribu kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Simba,DannyMrwanda ila kama itashindikana wataelekeza nguvu zao kwa Javu na Bahanuzi.

5.Shiboli asaini PolisiMorogoro inaelezwa kuwa mshambuliaji wa zamani wa Simba,KageraSugar amesaini na timu ya PolisiMorogoro baada ya kuachwa na CoastalUnion.

6.RamadhaniChombo"Redondo";Siondoki Azam FC,kiungo mchezeshaji wa Azam RamadhaniChombo amesema hatarajii kuondoka katika klabu hiyo huku akisema Azam mwakani itashiriki michuano ya CAF.

7.Simba yataja bei ya EmmanuelOkwi,Yanga yadai wanataka kumng'oa Msimbazi mshambuliaji huyo raia wa Uganda.Simba wasema ni dola 900000 zaidi ya bilioni moja za kitanzania

8.Azam FC;Tulishakamilisha usajili wetu msituhusishe na kusajili wachezaji wengine.

9.Coastal union;Usajili tuliofanya lazima tuchukue ubingwa msimuu ujao.Wasema lazima wacheze michuano ya kimataifa na kuiwakilisha nchi kimataifa,wazionya Simba na Yanga.

No comments:

Post a Comment